Quantcast
Channel: Strictly Gospel » NENO
Viewing all 33 articles
Browse latest View live

Nguvu ya ulimi

$
0
0

CK-BURKINA42

Biblia Takatifu inasema kuwa “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; nao waupendao watakula matunda yake.”

Ni kwa nini wana wa Mungu wanatumia ndimi zao kujiumbia mabaya, kushindwa, umaskini, kutokufanikiwa na mengine wasiyoyapenda ilhali wangaliweza kutumia ndimi hizohizo kutabiri, kukiri au kuumba kwa ajili ya mambo mazuri na ya mafanikio.

Je, inawezekana ukakutana na jambo gumu ukaliambia “wewe tatizo nakuambia utahama sasa!”?

Emmanuel


Filed under: NENO

Nia Zetu zifanywe upya

$
0
0

neno

Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu – Warumi 12: 2

Na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; – Waefeso 4: 23

Neno la Mungu linatukumbusha sisi tunaomwamini Bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wetu ya kwamba, ili tuweze kuishi maisha ya ushindi ni lazima tuendelee kufanywa upya katika roho za nia zetu kila siku, au kwa maneno mengine, mawazo na mitizamo yetu inabidi ibadilike kuendana na Neno la Mungu linavyosema. Tusikubali kuishi tena kama watu wasio na tumaini, Neno linatuambia ya kwamba Mungu anatutakia mema siku zote za maisha yetu ( Yeremia 29: 11, 3 Yohana 1: 2).

Labda nitoe mfano mmoja halisi; tuseme umekabiliwa na tatizo la ugonjwa, badala ya kuwaza na kusema kama wengine wasiomjua Mungu maneno kama vile “ugonjwa huu utaniua”, au “huu ni ugonjwa wangu”, au “kila mwaka lazima niugue hivi”, badili kauli yako ukatae huo ugonjwa na dalili zake zote ukikiri Neno linavyosema “kwa kupigwa kwake mimi nimepona”, “Jehovah Rapha, Bwana ndiye mponyaji wangu”. Kumbuka pia Bwana Yesu alitupa mamlaka akisema “waniaminio…wataweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya”.

Tunazo ahadi nyingi tu katika Neno la Mungu kuhusu uponyaji, mahitaji na mambo mbalimbali, yaamini na kuyakiri uushuhudie mkono wa Mungu maishani mwako! Kwa kifupi, kufanywa upya katika roho ya nia zetu, ni kitendo cha kudhamiria KULIAMINI Neno la Mungu KULIKO mazingira yetu. Tutambue ya kuwa Mungu si mwanadamu hata aseme uongo, hivyo basi Neno lake siku zote ni kweli (Warumi 3:4) na sisi tuna haki na kila ahadi kwa sababu ya kazi kamilifu ya ukombozi aliyoifanya Bwana Yesu pale msalabani.

Tuelewe ya kwamba sisi hatuko peke yetu tena, tunaye Roho Mtakatifu ndani yetu naye atatuwezesha kuliamini Neno linavyosema na kukubaliana nalo kuanzia kwenye mitazamo yetu, mioyo yetu na hatimaye kwenye kauli zetu na matendo yetu, ili tuishi maisha ya ushindi kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Amen!

Mbarikiwe watakatifu wa Bwana Yesu,

–Patrick

Filed under: NENO

Tusiipungukie Neema ya Mungu

$
0
0

amani

14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; 15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo. – Waebrania 12:14-15 SUV

Neno la Mungu linatuhimiza kutafuta kuwa na amani na watu wote kwa bidii tena bila kubagua, maana tukiishi kwa amani na wote wanaotuzunguka tutaweza kuwavuta kwa ushuhuda wa maisha yetu kwani sisi ni barua ya wazi inayosomwa na wote. Lengo kuu mojawapo la kuishi kwa amani na wote ni ili nao wapate fursa ya kuisikia Injili na kuokolewa, kwa maana tukiishi na majirani zetu kiugomvi ugomvi, kiukorofi ukorofi tutakosa ujasiri wa kuwashuhudia, licha ya kwamba tutawafanya waifunge mioyo yao washindwe kuipokea Injili toka kwetu.

Yatupasa kuishi maisha ya utakatifu. Utakatifu wa Mungu hatuupati kwa kujitahidi kwa juhudi zetu kuzishika zile amri kumi, la hasha. Katika zama hizi za Agano Jipya, baada ya Bwana Yesu kukamilisha kazi ya kutukomboa na kutupatanisha na Mungu, tunavikwa utakatifu na Mungu mwenyewe kwa Neema yake tunapomwamini Bwana Yesu kama Bwana na mwokozi wetu. Roho wa Mungu ndani yetu anatuongoza katika njia za Haki kwa ajili ya jina lake, anaiandika sheria yake mpya ndani yetu, sheria ya Roho wa Uzima (Romans 8:2) na amri mpya ya Upendo (Yohana 13:34, 1 Yohana 4:19 -21). Utakatifu tunaupata toka kwa Kristo mwenyewe, kwani yeye alifanyika kuwa dhambi ili sisi tuweze kufanyika kuwa Haki ya Mungu (2 Wakorintho 5:21). Ndani yake sisi tunafanyika kuwa wana wa Mungu, watakatifu, watu waliotengwa mahususi kwa ajili yake ili tupate kuzitangaza sifa zake. Utakatifu ulioko ndani yetu utadhihirika katika mienendo yetu iliyojaa upendo, furaha na amani katika Roho Mtakatifu, na wale wasiomjua Mungu wataweza kumwona na kumfahamu kupitia sisi.

Kuishi kwa amani na wote na kuwa na utakatifu vinawezekana pale tu tutakapohakikisha kuwa hatuipungukii Neema ya Mungu. Neema ya Mungu ni fadhila zake na wema wake ambao hatuustahili ila anatukirimia bila kikomo kwa sababu ya kazi kamilifu ya ukombozi aliyoifanya Bwana Yesu kwa kufa na kufufuka kwake. Katika Kristo tuna haki zote mbele za Mungu kama watoto wake wapendwa, tunao ujasiri wa kwenda mbele zake bila hofu, kwani dhambi zetu zilizotutenganisha naye Bwana Yesu alishazichukua zote katika mwili wake juu ya msalaba. Kwa hiyo leo hii vyote tunavyopokea maishani mwetu tukiwa ndani ya Kristo ni kwa Neema yake, siyo kwa jitihada zetu.

Tunapojaribu kupokea chochote toka kwa Baba kwa jitihada zetu wenyewe tukidhani zitatustahilisha mbele zake tunaipungukia Neema ya Mungu na matokeo yake shina la uchungu linaanza kuchipuka ndani yetu, hasa pale tuwaonapo wengine wakibarikiwa na kufanikiwa “kirahisi tu” bila kufunga sana na kukesha sana wakiomba sana kama sisi. Tafadhali nielewe, kufunga, kukesha na kuomba kuna nafasi yake, lakini kamwe siyo vigezo vya kutustahilisha kupokea chochote toka kwa Mungu leo hii. Vyote tunavyovihitaji kwa ajili ya maisha haya na utauwa leo hii viko ndani ya Kristo na tunavipata kwa kuzidi kumjua sana yeye aliyetuita kwa utukufu na wema wake (2 Petro 1:3). Ahadi zote za Mungu kwetu sisi tulio katika Kristo ni ndio nasi tunasema amina na kuzipokea!

Wapendwa tusiipungukie Neema ya Mungu na kuruhusu shina la uchungu lichipuke na kututia unajisi sisi wenyewe na wale wanaotuzunguka, na kama tunajikuta na hatia katika eneo hilo tusikubali adui atutese kwa kutujazia shutuma na hukumu tujione hatufai. Neno linasema ikiwa mioyo yetu inatuhukumu yeye ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote kwa hiyo basi tusiendelee kulea shina la uchungu mioyoni mwetu tutubu kwa kukiendea Kiti cha Rehema ili tupate Neema na Rehema ya kutusaidia wakati wa mahitaji. Mbarikiwe!

Kumbuka ya kuwa Baba yako wa mbinguni anakupenda sana na hataki ukose kupokea,kushiriki na kufurahia vyote alivyo navyo kwa ajili yako. Anayo makusudi mema na maisha yako. Mpendwa, Mungu yuko upande wako, hayuko kinyume nawe ndio maana anakuasa na kukutia moyo usiipungukie Neema yake. Kwa imani pokea wingi wa Neema na kipawa cha Haki upate kutawala pamoja Kristo (Warumi 5:17)

Mungu na azidi kuwabariki,

Patrick

 


Filed under: NENO

Tusijisumbue, Tuliamini Neno

$
0
0

biblia

6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. – Wafilipi 4:6-7 SUV

Neno la Mungu linatuambia hivi – tusijisumbue kwa jambo lolote – yaani tusiruhusu chochote kitufanye tuanze kusumbuka mioyoni mwetu tujikiulizauliza itakuwaje, tutafanyaje hadi kufikia hatua ya kukosa amani na kuruhusu hofu, mashaka, wasiwasi na woga viweke makao ndani yetu na kuanza kututesa. Tunalo Neno la Mungu, lililojaa ahadi zake kwetu na ahadi zake zote kwetu ni ndio na amina katika Kristo Yesu Bwana na Mwokozi wetu.

Tunapaswa kuleta haja zetu zote mbele za Mungu kwa njia ya sala na maombi tukiwa na mioyo iliyojaa shukurani kwani tunazo ahadi nyingi za ukuu, wema na utayari wa Mungu wetu kukutana na mahitaji yetu. Tukumbuke ni neema ya Mungu tu inayotuwezesha kupokea vyote Mungu alivyo navyo kwa ajili yetu tunapoliamini Neno lake Yeye aliyemtoa Mwanae kwa ajili yetu hatakosa kutukirimia vyote pamoja naye. Wapendwa, lazima tufikie mahali tuliamini Neno la Mungu kuliko tunavyoyaamini mazingira yetu.

Tunapoleta haja zetu mbele zake kwa imani tukiwa na mioyo ya shukrani, kwanza kabisa amani yake ipitayo fahamu zetu itatuhifadhi mioyo yetu na nia zetu na hivyo itatuepusha na hali ya kuwa na wasiwasi na kukosa amani, Ndio maana unaweza kumuona mtu anayemjua na kumwamini Mungu wake anapitia mambo magumu sana lakini amejaa furaha na amani tele, hanung’uniki, halalamiki wala hatumii yale anayoyapitia kama kisingizio cha kutafuta huruma za wanadamu. Ameshakabidhi yote mikononi mwa Mungu na anaamini kabisa ya kuwa Mungu amemsikia na ufumbuzi upo tayari, kwani analiamini Neno la Mungu.

huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. . – 1 Petro 5:7 SUV

Wapendwa, badala ya kuendelea kuhangaika na fadhaa zetu sisi wenyewe, tuitikie wito na ahadi ya Mungu kwetu. Tumtwike Yeye fadhaa zetu zote, Yeye Muumba wa vyote, Mwenye ufahamu wote na hekima yote kwa upendo  anatukaribisha tumtwike fadhaa zetu zote. Tuuitikie mwaliko huu wa Mungu wetu leo, tusiupuuzie.

Leo hii ujapo mbele za Baba yako wa Mbinguni, kumbuka ya kuwa ameahidi kukutana na kila hitaji lako tena anajishughulisha sana kwa mambo yako. Amani yake ipitayo akili zote itakuhifadhi moyo wako na nia yako katika Kristo Yesu usiyumbishwe na mashaka, hofu au wasiwasi. Na moyo wako unapokuwa umefunikwa na amani ya Mungu basi ni rahisi kwako kuisikia sauti yake akikuongoza na kukuelekeza hatua za kuchukua kupata ufumbuzi katika yale yanayokukabili.

Mzidi kubarikiwa na Bwana Yesu,

Patrick


Filed under: NENO

God’s Incredible Plan for You

$
0
0

“Just by understanding God’s love for you, and how He has felt about you from the beginning, and what He has wanted for you, begins to increase your faith and strength.

That is what it was designed to do as we see in Psalm 139:14-18. (NLT) “Thank you for making me so wonderfully complex! Your workmanship is marvelous—and how well I know it. You watched me as I was being formed in utter seclusion, as I was woven together in the dark of the womb. You saw me before I was born. Every day of my life was recorded in your book. Every moment was laid out before a single day had passed. How precious are your thoughts about me, O God! They are innumerable! I can’t even count them; they outnumber the grains of sand! And when I wake up in the morning, you are still with me!“

When you find out what God wants for you – what He intended for you – and that He is not out to condemn you but to strengthen your life to become a world changer, your life begins to take new shape. Strength from God comes to your life. How do you open the door to this strength so that it continues to come and so that you feel and see it begin to change you?  What is the first secret to tapping into the power and then plan of God for this significant life? It’s putting these truths in your mouth! That is a God secret that He wants you to know! It’s powerful. It’s life-changing.

God spoke through Isaiah to help us take hold of this powerful truth saying, “And this is my covenant with them,” says the Lord. “My Spirit will not leave them, and neither will these words I have given you. They will be on your lips and on the lips of your children and your children’s children forever. I, the Lord, have spoken!  Isaiah 59:21 (NLT)

Begin now by getting in front of a mirror and saying, “Thank you Lord. You have made me wonderfully complex! Your workmanship concerning me is marvelous and I now know it. You watched me as I was being formed and prepared my days and your plan for my life before I ever lived one day. It’s time I started living by your strength and power instead of mine own. I thank you for helping me to grow in your strength and power every day. I thank you that your thoughts about me are kind and empowering and your plan and desire for me even more precious. I thank you that you are with me now and forever. These are your words and I have and will continue to put them in my mouth and on my lips until they instinctively flow from my heart. Thank you for Jesus and making all this available to me through Your love and sacrifice for me. I am strengthened in you today. In Jesus name Amen!”

These are God’s Words about you. Write God’s covenant promises down as you see them in the Bible. Put them in your mouth and speak them each day until they begin to sink in. You are honoring God in doing so. You are exercising your faith! You will begin to experience a new level of the power of God and His strength in your life. It will thrill your heart!

 Psalms 19:14 (NLT) “May the words of my mouth and the meditation of my heart be pleasing to you, O Lord, my rock and my redeemer.”

 In His Love,

Pastor Tim Burt


Filed under: NENO

Najivunia kuwa raia wa mbinguni!!

$
0
0

 neno

Ukiwa Mmarekani, Serikali Ya Marekani Itafanya Chochote Kukulinda Ama Kuhakikisha Usalama Wako… Ikitokea Adui Akamgusa Mmarekani Au Kumdhuru, Serikali Ya Marekani Huwa Hailichukulii Kwa Urahisi Jambo Kama Hilo…

Sipati Picha Ukiwa Mkristo, Raia Wa Serikali Ya Mbinguni; Mungu, Rais Wa Serikali Ya Mbinguni Anakuwa Ukuta Wa Moto Kukuzunguka Na Utukufu Ndani Yako, Anakuzunguka Kama Milima Iizungukavyo Yerusalemu, Anakuwa Adui Wa Adui Zako, Anakuwa Ngome, Kimbilio, Msaada Na Nguvu Zako… Huhitaji GPS Kwa Ajili Ya Kuku-locate; Amekuchora Kwenye Kiganja Chake, Kuta Zako Zi Mbele Zake Daima, Jicho Lake Linazungukazunguka Duniani Ili Ajionyeshe Mwenye Nguvu Kwa Ajili Yako, Anakupa Fursa Ya Kuwa Mrithi Pamoja Na Kristo, Anakuhakikishia Kukupatia Hazina Za Gizani Na Kukupa Kabila Za Watu Kwa Ajili Ya Maisha Yako, Anakuhakikishia Kustawi Mjini Na Mashambani, Anakufungulia Mlango Wa Mafanikio Kwa Kila Ulifanyalo Sawa Na Mti Uliopandwa Kando Ya Vijito Vya Maji, Anakupa Uhakika Wa Kuwa Juu Tu Na Wala Sio Chini… Anakupa Access Ya Kufanya Mawasiliano Moja Kwa Moja Na Yeye Kupitia MTANDAO Huitwa JINA LA YESU, Ambao Unakuhakikishia Kushughulikiwa Kwa Hitaji Lako!

Haiishii Hapo, Anakuwekea Majeshi Ya Malaika Ili Wakulinde Na Kukuokoa, Na Anawaagiza Wakuongoze Hadi Mahali Alipokutengenezea, Wanakuwa Pamoja Nawe Muda Wote Maana Hao Ni Watumishi Wako Wewe Utakayeurithi Uzima Wa Milele!

Kubwa Zaidi, Unao UZIMA WA MILELE; Aina Ya Uzima Alionao Mungu, Unaokupa Tiketi Ya Kufanya Vitu Kwa Kiwango Cha Mungu…Kwa Leo Inatosha Mwanafunzi Wangu Mwema!

AM PROUD TO BE A CHRISTIAN; THE CITIZEN OF HEAVEN AND THE AMBASSADOR OF CHRIST ON EARTH! 

–Conrad Conwell

Filed under: NENO

Tuwe Makini na tunayoongea

$
0
0
methali

Tuwe makini na kila tunachoongea kwa sababu:

Mithali 6:2 Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,

Mithali 12:18 Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya

Waefeso 4:29 Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.

Yakobo 3:5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

Mhubiri 5:6 Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?

Mhubiri 5:2 Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache.

Ongea mazuri kwa sababu:
Mithali 13:2 Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake; Bali nafsi ya mtu haini itakula jeuri.

Mithali 16:21 Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara; Utamu wa maneno huongeza elimu.

Mithali 16:24 Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.

Mithali 18:4 Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi; Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.

Mithali 18:20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake.

Mithali 18:21 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.

1Petro 3:10 Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.

Wakolosai 4:6 Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.

Zaburi 119:105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Unachojaza moyoni ndicho unachokisema:
Luka 6:45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.

Linda moyo wako:
Mithali 4:23 Mithali 4:23. Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Moyo unalindwaje?
Wakolosai 3:16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

Kwa sababu:
Mathayo 12:34b Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.

Mathayo 12:36 Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.

Mathayo 12:37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.

Ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu(Mwanzo1):
Waebrania 11:3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.

Kwa neno unaloamini na kulisema waweza badili ulimwengu wako:
Marko 11:23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake.

Maneno yako yawe machache, ukiwaza mabaya jizuie usiseme:
Mithali 17:28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Mathayo 5:37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.

Kutoka 4:12 Basi sasa, enenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na kukufundisha utakalolinena.

Mithali 30:32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.

Ayubu 15:6 Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi; Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.

–Silva Giga


Filed under: NENO

Hekima hujenga, upumbavu hubomoa huku ikiona ipo sawa.!!

$
0
0

pst

MIT. 14:1 SUV

Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

Hamna wakati ambapo upumbavu unakuwa kileleni kama wakati mtu akiwa na hasira.

MHU. 7:9 SUV

Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.

Unapokuwa na hasira unakuwa kwa kipindi hicho umejawa na upumbavu kifuani. Unaweza ukasukuma maneno toka kifuani yatakuwa maneno ya upumbavu tu. Ni vema ungenyamaza kimya.

MIT. 17:28 SUV

Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Katika hasira yako ukiamua kufanya jambo japo litakuwa la kipumbavu lakini wewe kwa sababu ya hasira yako utakuwa unaliona sawa tu.

MIT. 12:15 SUV

Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.

Hasira na hasara hazijapishana sana. Tofauti yake ni herufi moja tu.

–Pastor Carlos Kirimbai


Filed under: NENO

The Inspirational Thought Of The Day:

$
0
0

“With God and the knowledge of His Word inside of you, nothing is impossible for you.” 


Filed under: NENO

Mpende adui yako!

$
0
0

mlk

‘‘Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Mpende jirani yako na umchukie adui yako.’ Lakini mimi ninawaambia, Wapendeni adui zenu na waombeeni wanaowatesa ninyi, ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana Yeye huwaangazia jua lake watu waovu na watu wema, naye huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. Kama mkiwapenda wale wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani? Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo?

Mathayo 5:43-46


Filed under: NENO

KUTIMILIZA TORATI

$
0
0

 

law2

 

UTANGULIZI

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nawe mdau wa SG. Tunaishi katika kipindi ambacho kuna namna nyingi za injili, na usipokuwa makini unaweza kufikiri kuwa uko katika injili ya Yesu Kristo kumbe mtu ulishahama – kwa wale wanamuziki, wanasema umetoka “nje ya key”! Hata enzi za Kanisa la kwanza, jambo kama hili lilipata kutokea kule Galatia (soma Wagalatia 1:6-9).

Ukisoma Mathayo 5:20 unakutana na maneno haya toka katika kinywa cha Bwana wetu Yesu Kristo:

“Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.”

Andiko hili limekuwa likitumiwa na wengi kusisitiza kwamba, ili kuingia ufalme wa mbinguni hatuna budi kufanya matendo mema au mazuri na mengi zaidi ya vile ambavyo mafarisayo walikuwa wanafanya. Je mafarisayo walikuwa wanafanya nini?

“Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.” (Luka 18:11-12)

Hivyo, hoja hiyo husisitiza, tunapaswa kufunga zaidi ya mafarisayo na kutoa zaka na kufanya mambo mengine zaidi yao vinginevyo haki yetu haitazidi ile haki ya mafarisayo na hivyo hatutaweza kuingia ufalme wa mbinguni.

Je, ni kweli Bwana Yesu alimaanisha hivyo? Twende pamoja. Kanuni yetu, kama kawaida, ni kujenga hoja na kujadili kwa kuzingatia kile ambacho Maandiko Matakatifu yanasema.

BWANA YESU NA TORATI

Ili kuelewa ujumbe wa Bwana Yesu alipowaambia watu waliokuwa wakimsikiliza kuwa haki yao isipozidi ya mafarisayo hawataingia katika ufalme wa mbinguni, inabidi kusoma mstari huo katika muktadha wake.

“Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali KUTIMILIZA. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata YOTE YATIMIE. Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu ISIPOZIDI hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, USIUE, na mtu akiua, itampasa hukumu. Bali mimi nawaambieni, Kila AMWONEAYE ndugu yake HASIRA itampasa hukumu; na mtu AKIMFYOLEA ndugu yake, itampasa baraza; na mtu AKIMWAPIZA, itampasa jehanum ya moto.” (Mathayo 5:17-22, SUV, msisitizo wangu)

Yesu alikuwa akiongea na makutano (Mathayo 5:1), katika kipindi ambacho torati ilikuwa imeshika hatamu maana bado kilikuwa ni kipindi cha agano la kale. [Kuzungumzia kwa undani maswala ya agano la kale na lile jipya haiko katika lengo (scope) la mjadala huu, ila kwa ufupi sana niseme tu kuwa agano la kale Mungu aliliweka na wana wa Israeli pale alipowatoa kule Misri (soma Waebrania 8:8-9), na katika kipindi hicho wana wa Israeli walipewa torati waishi kwa hiyo. Agano jipya lilikuja kuanza Bwana Yesu alipotolewa dhabihu pale msalabani (soma Waebrania 9:11-15).] Bwana Yesu aliweka bayana kuwa alikuwa amekuja duniani “kutimiliza” torati. Je “kutimiliza” huku kulikuwa ni kufanya nini hasa, na hayo “yote” ambayo Yesu alisema kwamba yalikuwa hayana budi “kutimia” yalikuwa ni yapi?

Yesu alikuja KUTIMILIZA yale YOTE yaliyokuwa yamenenwa na torati na manabii. Yesu alilifafanua jambo hilo kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka maana katika kitambo chote alichokuwa nao hawakumwelewa.

“Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu NILIYOWAAMBIA nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba NI LAZIMA YATIMIZWE YOTE niliyoandikiwa katika TORATI YA MUSA, na katika MANABII na ZABURI. Ndipo AKAWAFUNULIA AKILI ZAO wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, NDIVYO ILIVYOANDIKWA, KWAMBA KRISTO ATATESWA NA KUFUFUKA SIKU YA TATU; na kwamba MATAIFA YOTE WATAHUBIRIWA KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI, kuanza tangu Yerusalemu.” (Luka 24:44-47, SUV, msisitizo wangu)

Kwa hivyo, Yesu aliposema kuwa hakuja kuitangua torati na manabii bali kuitimiliza, alikuwa anamaanisha kuwa alikuwa amekuja duniani ili YALE YOTE YALIYOTABIRIWA katika torati na manabii kuhusu kuteswa, kufa na kufufuka kwake, na hatimaye injili ihubiriwe duniani kote YATIMIE. Ni vema tukumbuke kuwa torati ilikuwa ni kiongozi wa kutuleta kwa Yesu Kristo, maana tunasoma, “Lakini KABLA ya kuja ile IMANI tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa. Hivyo TORATI IMEKUWA KIONGOZI kutuleta kwa Kristo, ILI TUHESABIWE HAKI KWA IMANI. Lakini, IWAPO IMANI IMEKUJA, HATUPO TENA CHINI YA KIONGOZI.” (Wagalatia 3:23-25, SUV, msisitizo wangu)

HAKI YA MAFARISAYO NA HAKI ANAYOITAKA MUNGU KWETU

Baada ya kuona kile ambacho Bwana Yesu alimaanisha aliposema kuwa hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza, tunaweza sasa kuelewa kile alichomaanisha alipozungumzia kuwa haki ya mtu inapaswa kuizidi ile ya mafarisayo ili kuingia katika ufalme wa mbinguni. Neno lililotafsiriwa kama “haki” katika Mathayo 5:20 limetokana na neno la Kiyunani “dikaiosune¯” linalomaanisha “the character or quality of being right or just”, yaani, ile hali au tabia ya kuwa sawa (bila kosa lolote) au mwenye haki.

Tafsiri ya Kiingereza ambayo inafafanua zaidi maana za maneno inasema:

“For I tell you, unless your righteousness (your uprightness and your right standing with God) is more than that of the scribes and Pharisees, you will never enter the kingdom of heaven” (Matthew 5:20, Amplified)

Mafarisayo na waandishi walikuwa wakijihesabia haki (yaani, walijihesabu kuwa wako sawa) mbele za Mungu kwa kujipima ni kwa jinsi gani walikuwa wanafanya yaliyoandikwa katika torati. Ndio maana tunasoma:

“Akawaambia mfano huu watu WALIOJIKINAI YA KUWA WAO NI WENYE HAKI, WAKIWADHARAU WENGINE WOTE. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa MIMI SI KAMA WATU WENGINE, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza shuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, HUYU ALISHUKA KWENDA NYUMBANI KWAKE AMEHESABIWA HAKI KULIKO YULE; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.” (Luka 18:9-14, SUV, msisitizo wangu)

Bwana Yesu katika hotuba yake ya mlimani alifafanua kuwa, katika torati iliandikwa “usiue” (yaani wasifanye tendo ambalo linaonekana kwa macho – kuua – na ambalo lilikuwa limeandikwa katika torati) lakini yeye akawatajia mambo ambayo mtu akiyafanya itampasa adhabu – kumwonea hasira mwenzake, kumfyolea, au kumwapiza. Hayo aliyowatajia hayakuandikwa katika torati yao, lakini yalikuwa ni mwanzo wa hasira ambayo mtu anakuwa nayo kabla ya kufikia hatua ya kumwua mwenzake. Nitatoa mfano mwingine.

“Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.” (Mathayo 5:27-28, SUV)

Yesu aliwaambia mafarisayo waliokuwa wakijihesabia haki kwa kuwa hawakuzini kwamba, hata kama hawakuzini lakini kama waliwaangalia wanawake kwa kuwatamani kingono tayari walikuwa wamezini nao. Tamaa ya kutaka kufanya ngono na mwanamke ndiyo hupelekea mtu kutafuta fursa ya kuzini naye (soma pia Yakobo 1:13-15). Mafarisayo walijihesabia haki kwa kuwa hawakufanya lile tendo la ngono, lakini Yesu akawasisitizia kuwa kutamani kufanya ngono na mwanamke – hata bila ya kufanya tendo lenyewe – tayari ilikuwa ni uzinzi.

Kupitia mifano hiyo, Bwana Yesu alikuwa anawaeleza kiwango cha juu cha haki ambacho Mungu alikuwa anakitarajia kwa wanadamu – si tu kufuata vile torati ilivyokuwa ikisema (usiue, usizini, usiibe, nk), bali kwenda kushughulikia kwenye MZIZI wa hayo maovu, yaani kwenye moyo ambako mawazo ya kufanya maovu hayo huanzia. Huko kukishashughulikiwa, mtu hatahitaji tena kuwa na orodha ya mambo ya kutokufanya bali atajikuta anaenenda katika njia iliyo sawa na hafanyi yasiyopasa. Kwa maneno mengine, Yesu alikuwa anawaeleza namna ya haki ambayo ilikuwa ni ya KIWANGO CHA JUU, iliyozidi kwa mbali sana namna ile ya haki ambayo mafarisayo walikuwa wanajihesabia.

Mahali pengine Yesu aliwaambia mafarisayo, ambao walijihesabu kuwa ni wenye haki mbele za Mungu kwa zile jitihada zao za kutii torati (japo walichanganya na mapokeo yao ambayo hayakuwemo katika torati (angalia, kwa mfano, Mathayo 15:6)), maneno haya:

“Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya MIOYO ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. Haya yote yaliyo maovu YATOKA NDANI, nayo yamtia mtu unajisi.” (Marko 7:20-23, SUV, msisitizo wangu)

Mafarisayo walijihesabia haki kwa kujitahidi kukwepa kufanya matendo maovu na kufanya matendo mema yanayoonekana (angalia Mathayo 6:1-6), lakini Yesu aliweka bayana kwao kuwa walitakiwa kushughulika na mioyo yao ambako matendo yote huanzia huko. Ndiyo maana aliwaambia:

“Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa MNASAFISHA NJE ya kikombe na chano, na NDANI YAKE vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi. Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza NDANI ya kikombe, ILI NJE YAKE NAYO IPATE KUWA SAFI.” (Mathayo 23:25-26, SUV, msisitizo wangu)

Kama haki ya mtu itaishia katika kutii torati au orodha ya makatazo (prohibitions), kwamba usifanye hiki au kile, itakuwa sawa na ile waliyojihesabia mafarisayo na waandishi. Hiyo haitasaidia kitu.

“Basi ikiwa MLIKUFA PAMOJA NA KRISTO mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, KWA NINI KUJITIA CHINI YA AMRI, kama wenye kuishi duniani, Msishike, msionje, msiguse; (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata MAAGIZO NA MAFUNDISHO YA WANADAMU? Mambo hayo YANAONEKANA KANA KWAMBA YANA HEKIMA, katika namna ya IBADA MLIYOJITUNGIA WENYEWE, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini HAYAFAI KITU kwa kuzizuia tamaa za mwili.” (Wakolosai 2:20-23, SUV, msisitizo wangu)

Haki yetu inatakiwa izidi hiyo – itokane na kushughulikia kule ndani kabisa, kwenye moyo, ambako maovu huanzia. Na hilo haliwezekani pasipo kumpokea Kristo Yesu na kuzaliwa upya, na kujifunza kuongozwa na Roho Mtakatifu katika kufisha mwili pamoja na tamaa zake.

“Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.” (Wagalatia 5:24)

NAFASI YA MATENDO MEMA

Baada ya kusema hayo, hebu tuangalie nafasi ya matendo mema katika maisha ya mtu aliyemwamini Kristo Yesu.

Ni muhimu kutambua kuwa Mungu alituumba ili tutende yaliyo mema kwa wengine:

“Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende MATENDO MEMA, ambayo TOKEA AWALI MUNGU ALIYATENGENEZA ILI TUENENDE NAYO.” (Waefeso 2:10, SUV, msisitizo wangu)

Kama wana wa Mungu, tunatarajiwa kufanya yaliyo mema (soma pia Mathayo 5:16, 1 Timotheo 2:8-10, Tito 2:7-14; 3:14), lakini SI MATENDO HAYO yanayotufanya tuhesabiwe haki mbele za Mungu (angalia Warumi 3:23-24, Waefeso 2:8-9, Warumi 11:6, Wagalatia 2:21, ). Tukitarajia au kutafuta kuhesabiwa haki kwa sababu ya matendo yetu mema tunarudi kule kwenye torati na kuachana na neema.

Matendo mema tunayoyatenda ni matunda ya mabadiliko yanayotokana na utendaji au uhai wa ile imani katika Kristo Yesu iliyo ndani yetu. Ndiyo maana Yakobo aliandika:

“Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki, na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini? Vivyo hivyo na imani, ISIPOKUWA INA MATENDO, IMEKUFA NAFSINI MWAKE. Lakini mtu atasema, Wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami NITAKUONYESHA IMANI YANGU KWA NJIA YA MATENDO YANGU.” (Yakobo 2:14-18, SUV, msisitizo wangu)

Uhai wa imani yetu katika Kristo Yesu unaonekana kwa nje kupitia matendo yetu. Kama hakuna mabadiliko, Maandiko yako wazi kabisa kuwa imani hiyo imekufa.

KWA KUMALIZIA

Nisisitize kuwa, Bwana Yesu alikuja duniani akafa msalabani na kupata mateso mengi, damu yake ikamwagika, ili ashughulikie mzizi wa dhambi unaotufanya tuwaze na hatimaye kutenda maovu. Kama tutang’ang’ania kutaka kuishi kwa kufuata mlolongo wa sheria na kujihesabia haki kwa umahiri wetu wa kuzifuata, tutakuwa tumetoka nje ya mstari na kuifanya kazi yote ya Mwokozi kuwa haina maana. Tunapomwamini, imani ile inapotenda kazi ndani yetu inapelekea sisi kutenda matendo mema yanayoonekana kwa nje na kudhihirisha badiliko lililotokea katika maisha yetu.

Mungu wa mbinguni akubariki.

Joel Msella


Filed under: NENO

Mungu bado anachukukia vitu vifuatavyo!!

$
0
0

“Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; moyo uwazayo mawazo mabaya; miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitna kati ya ndugu”

–Mithali 6:16-19


Filed under: INJILI, NENO

Lijue Neno kwa ajili yako Mwenyewe!

$
0
0

biblia

Jitahidi (Jifunze) ili kujionesha kuwa umekubaliwa na Mungu,  mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa usahihi Neno la kweli (2 Timotheo 2:15),

Kwa wewe kuishi maisha ya furaha, na kuwa udhihirisho kamilifu wa mapenzi, haki, na utukufu wa Mungu, unatakiwa kulijua Neno wewe mwenyewe na kuishi kwa Neno. Wale wasiolijua Neno la Mungu ni kwa tabu sana wanaweza timiza ile shauku na mipango ya Mungu katika maisha yao. Neno la Mungu lilikufanya wewe (1 Petro 1:23), hivyo usipoishi kwa Neno, hautokuwa yule “wewe” Mungu aliyemtazamia, wala hautotimiza hatma Yake Kwako. Hii ndio sababu tunafundisha Neno na kuwatia moyo watoto wa Mungu kuwa wanafunzi wa Neno. Ni lazima ulijue Neno kwa ajili yako mwenyewe (lijue wewe mwenyewe).

 Usiishi katika viwango vya kudhania.  Usiache watu wakuhamasishe (wakushawishi) na mitazamo yao ya “kidini” kuhusu Mungu. Usikubali kwamba kitu fulani kinatoka kwa Mungu kwa sababu tu kinasikika kama chema, kizuri ama cha kidini.

Yesu Alisema katika Yohana 5:39, “Chunguzeni maandiko…” ; Paulo alisema katika 2 Timotheo 2:15, “Jitahidi (Jifunze) ili kujionesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukilitumia kwa usahihi Neno la kweli.” Neno la Mungu ni ufahamu wa Mungu uliodhihirishwa; ni mapenzi Yake katika maandishi na yaliyoelezewa kwa ajili yetu. Ni faida ya ajabu namna gani hii, kwamba unaweza jifunza Neno wewe mwenyewe, ukalielewa, na kuliishi! Ni baraka kuu.

Kipimo cha maisha yako ya kitukufu na ushindi kitakua ni, kiwango gani cha maanifa ya Mungu unacho, na ni kiasi gani unakitendea kazi. Si umekuwa Mkristo muda mrefu kiasi gani; bali ni unajua Neno vizuri kiasi gani na kulitumia. Shukurani kwa Mungu tunayo faida isiyolinganishwa ya uwepo wa Roho Mtakatifu ukaaoa ndani yetu, Ambaye Hutupatia uelewa wa Neno! Yeye Ndiye mtunzi wa maandiko; hivyo unapojifunza, unaweza kumtegemea Yeye ili kukuongoza, na kukupatia kuona katika mafumbo na siri za ki-Ungu.

 Lipatie Neno umakini na muda wako. Jifunze na uliwekee moyo wako. Kama unataka kuishi maisha yaliyopita ukawaida, ni kwa Neno, kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu.

Imetafsiriwa kutoka kwa Mchungaji Chris Oyakhilahome


Filed under: NENO
Viewing all 33 articles
Browse latest View live