MIT. 14:1 SUV
Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Hamna wakati ambapo upumbavu unakuwa kileleni kama wakati mtu akiwa na hasira.
MHU. 7:9 SUV
Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Unapokuwa na hasira unakuwa kwa kipindi hicho umejawa na upumbavu kifuani. Unaweza ukasukuma maneno toka kifuani yatakuwa maneno ya upumbavu tu. Ni vema ungenyamaza kimya.
MIT. 17:28 SUV
Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.
Katika hasira yako ukiamua kufanya jambo japo litakuwa la kipumbavu lakini wewe kwa sababu ya hasira yako utakuwa unaliona sawa tu.
MIT. 12:15 SUV
Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
Hasira na hasara hazijapishana sana. Tofauti yake ni herufi moja tu.
–Pastor Carlos Kirimbai
Filed under: NENO
